Kikao cha usomaji wa Qur’ani tukufu katika kuhitimisha siku ya kwanza ya kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu Shahada.

Maoni katika picha
Miongoni mwa ratiba ya siku ya kwanza katika kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu Shahada ya kumi na tano linalo fanywa chini ya kauli mbiu isemayo: (Imamu Hussein –a.s- ni mnara wa umma na suluhisho madhubuti), kisomo cha kwanza cha Qur’ani kimefanyika ndani ya uwanja wa haram ya Abu Abdillahi Hussein (a.s) jioni ya Jumanne, (3 Shabani 1440h) sawa na (9 April 2019m).

Kikao hilifunguliwa na msomaji wa Atabatu Husseiniyya tukufu bwana Osama Karbalai, kisha kikafuata kikosi cha wasomaji wa Qur,ani kutoka Atabatu Husseiniyya tukufu tawi la Ahwaaz, walikua wanaburudisha masikio ya wahudhuriaji baina ya kusoma Qur’ani tukufu na Kaswida, kisha ikaendelea Darul Qur’ani ya Atabatu Husseiniyya tukufu, kupitia mmoja wa wanafunzi wake aitwae Hussein Hajjaar, aliburudisha wahudhuriaji kwa kisomo murua, halafu ukaingia wakati wa Atabatu Radhawiyya tukufu kutoka Jamhuri ya kiislamu ya Iran, akasoma Hamiid Shaakir Najaad, na kuhitimisha kwa kisomo cha Mmisri Hamdi Rashidi.

Kuhusu ratiba hii tumeongea na kiongozi wa idara ya habari ya Darul Qur’ani tukufu katika Atabatu Husseiniyya Ustadh Swafaa Silaawi, akasema kua: “Darul Qur’ani tukufu chini ya Atabatu Husseiniyya inatilia manani kufanya kikao hiki kila mwaka, katika ratiba ya kongamano la Rabiu Shahada, na huwakaribisha wasomaji bora wa kitaifa na kimataifa”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: