Katika malalo ya Imamu Hussein (a.s) na mbele ya kaburi lake takatifu: Makabila na Dini tofauti zinaonyesha mapenzi yao kwake.

Maoni katika picha
Baada ya kuchomoza jua la Alkhamisi la mwezi tano Shabani, kufuatia kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Imamu Zainul-Aabidina, miongoni mwa vipengele vya kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu Shahada awamu ya kumi na tano linalo endelea hivi sasa ni vitendo vya kiibada, wageni wa kongamano waliokuja kutoka mataifa mbalimbali na Dini tofauti wamesimama kwa heshima na unyenyekevu mbele ya kaburi la Imamu Hussein (a.s) na kusoma ziara yake tukufu na kutoa miito ya kiimani.

Baada ya kusimama watumishi wa Abu Abdillahi Hussein (a.s) na wageni wa kongamano ikasomwa Quráni tukufu ya ufunguzi na surat Fat-ha kwa ajili ya kuwarehemu mashahidi watukufu, baada ya hapo wakaelekea katika kaburi la bwana wa mashahidi (a.s) kufanya ziara na kutoa miito ya Imani iliyo kua ikisema:

Wito wa Aqida kwa walio changanikiwa ….. Hussein Hussein Hussein Hussein

Mbainishaji wa ujumbe wa Mitume na Manabii …… katunzwa na watawala wa Karbala

Zikafuatia kaswida za kidini.

Tukio hili la kiibada limepongezwa na kusifiwa na wageni wa kongamano, nalo hufanywa kila siku katika muda wa kazi baina ya zamu mbili ya asubuhi na jioni, kwa ajili ya kuhuisha utiifu kwa Imamu Hussein (a.s) pamoja na kujikumbusha malengo makuu yaliyo sababisha ajitolee damu na roho yake, ambayo ni uislamu na kufatwa sharia zake tukufu pamoja na mwenendo wa Mtume Muhammad (s.a.w.w).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: