Kongamano la Rabiu Shahada lahitimisha vikao vya uwasilishaji wa mada za kitafiti.

Maoni katika picha
Alasiri ya leo (5 Shabani 1440h) sawa na (11 April 2019m) kimefanywa kikao cha nne na cha mwisho cha uwasilishaji wa mada za kitafiti katika kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu Shahada ndani ya ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) katika Atabatu Abbasiyya, chini ya kauli mbiu isemayo: (Imamu Hussein –a.s- ni mnara wa umma na suluhisho madhubuti) na kuhudhuriwa na watafiti pamoja na wasomi mbalimbali kutoka nchi tofauti.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na katibu mkuu wa Atabatu Husseiniyya Sayyid Jafari Mussawiy (d.t) pamoja na jopo la wajumbe wa kamati kuu ya uongozi ya Atabatu Abbasiyya, kilifunguliwa kwa Quráni tukufu, halafu ikasomwa surat Fat-ha kwa ajili ya kuwarehemu mashahidi wa Iraq, kisha ikaanza kuwasilishwa mihtasari ya mada za kitafiti kama ifuatavyo:

Utafiti wa kwanza ulikua wa Shekh Iswamul Hamdi/ kutoka Yemen, utafiti wake unasema: (Riwaya za utukufu wa Imamu Hussein –a.s- kutoka kwa Maimamu watakasifu).

Utafiti wa pili ulikua wa Shekh Muslim Radhwai/ kutoka Afghanistani, utafiti wake unasema: (Utafiti wa kifiqhi katika vitabu vya Maqtal Husseini.. kitabu cha Iksiri Ibadaat cha Darbandi kama mfano).

Utafiti wa tatu ulikua wa Dokta Haidari Masjidi/ kutoka Iran, utafiti wake unasema: (Utafiti mpya katika riwaya za tahriif).

Wahudhuriaji walitoa maoni na michango mbalimbali, baada ya hapo watafiti walio shiriki katika kikao hiki wakapewa zawadi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: