Mgahawa wa Atabatu Abbasiyya tukufu umegawa makumi ya vyakula.

Maoni katika picha
Kutokana na kuingia mwezi wa Shabani mtukufu na kuongezeka kwa watu wanaokuja Karbala kuhuisha kuzaliwa kwa watu watukufu, mgahawa (mudhifu) wa Abulfadhil Abbasi (a.s) umegawa makumi ya vyakula kwa mazuwaru, chini ya utaratibu maalum wa kugawa chakula kwa mazuwaru.

Kama kawaida katika siku za ziaya hufunguliwa madirisha ya nje kwa ajili ya kugawia chakula, kutokana na ongezeko kubwa la watu amboa hujaa kwa ajili ya kupata chakula cha baraka itokayo kwa mnyweshaji wenye kiu Karbala, pia chakula hutolewa mchana baada ya Dhuhuraini, muda huo idadi kubwa ya mazuwaru huhitaji chakula, chakula hutolewa kutokana na wingi wa mazuwaru.

Fahamu kua mgahawa (mudhifu) wa Abulfadhil Abbasi (a.s) hutoa chakula kila siku kwa mazuwaru wa Atabatu Abbasiyya, na katika siku za ziara maalum hufungua madirisha ya nje kwa ajili ya kugawa chakula kwa mazuwaru wengi zaidi na kuwafanya wapate baraka za chakula cha mwenye malalo hii takatifu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: