Kitengo kinacho simamia eneo la katikati na haram mbili tukufu kimetumia uwezo wake wote katika kuwahudumia mazuwaru.

Maoni katika picha
Kama kawaida kitengo kinacho simamia eneo la katikati ya haram mbili tukufu chini ya Atabatu Husseiniyya na Abbasiyya, kimetumia nguvu zote katika kuwahudumia mazuwaru wa bwana wa mashahidi na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s), kwa ajili ya kuwarahisishia kukaa katika uwanja wa eneo la katikati ya haram mbili na kurahisisha matembezi yao kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Kazi zilizo fanywa na kitengo hicho katika siku za ziara ya nusu ya mwezi wa Shabani na kuzaliwa kwa Imamu Mahdi (a.f) kupitia idara zake zote ni hizi zifuatazo:

  • 1- Kutoa huduma ya habari kwa wanahabari wote waliopenda kurusha matukio ya ziara ya Shaabaniyya kutoka katika uwanja wa eneo la katikati ya haram mbili.
  • 2- Kuimarisha ulinzi na usalama kwa kushirikiana na kitengo cha kulinda nidham pamoja na walinzi wa haram mbili tukufu.
  • 3- Kutoa gari za usafi kwa vituo vya usalama pamoja na gari za maji, na kugawa maji kwa mawakibu na mazuwaru.
  • 4- Kutandika mazulia kwa ajili ya swala za jamaa na kupumzika mazuwaru.
  • 5- Kuhakikisha taa zinawaka vizuri usiku mzima kwa kiasi ambacho zinaakisi furaha ya tukio hili.
  • 6- Kuandaa mimbari kwa ajili ya vikao maalumu vya kusherehekea kuzaliwa kwa Imamu Mahadi (a.f).

Fahamu kua kitengo kinacho simamia eneo la katikati ya haram mbili tukufu pamoja na huduma hizo, kimetoa huduma ya maelekezo ya kidini kupitia vipaza sauti vilivyo enea katika uwanja huo.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: