Kitengo cha habari na utamaduni kinatangaza mashindano la filamu fupi kuhusu kongamano la nne la fatwa ya kujilinda.

Maoni katika picha
Kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu kinatoa wito kwa watu wote walio shiriki kuandika filamu, washiriki katika shindano la pili la filamu fupi bora kuhusu wanajeshi na Hashdi Shaábi, litakalo fanyika katika kongamano la kumbukumbu ya nne ya fatwa tukufu ya kujilinda, chini ya utaratibu ufuatao:

  • 1- Fikra ya filamu iendane na kauli mbiu ya kongamano.
  • 2- Filamu ionyeshe ushujaa wa wanajeshi na hashdi Shaábi katika kulinda taifa, misingi ya ubinaadam, mazingira na maeneo matakatifu kwa ujumla bila kuelemea upande wowote.
  • 3- Isiwe imeshawahi kuonyeshwa mitandaoni au kushiriki katika shindano lingine.
  • 4- Iwekwe kwenye (CD) na kukabidhiwa kwenye kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu pamoja na wasifu (cv) ya mtengenezaji wa filamu, au utumwe kwa barua pepe kwa anuani hii: alkafeelkids@gmail.com
  • 5- Mwisho wa kupokea filam zitakazo shiriki ni (10 Juni 2019m).
  • 6- Filamu isiwe chini ya dakika (3) na isizidi dakika (5).
  • 7- Matukio ya ukatili na umwagaji wa damu yasionyeshwe wazi bali yawekewe pazia.

Kumbuka kua washindi watano wa kwanza watazawadiwa kiasi cha (400,000) dinari laki nne za Iraq kila mmoja.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: