Kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinaadamu chaandaa masomo ya elimu rijali na maarifa ya sanadi.

Maoni katika picha
Katika mwendelezo wa kozi zake za uhakiki, uhadhiri, lugha ya kiarabu na mengineyo, kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinaadamu cha Atabatu Abbasiyya tukufu kimeandaa kozi iitwayo: (Ilmu rijali na maarifa ya sanadi), katika ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) ndani ya Ataba tukufu, kwa muda wa siku kumi na mbili, kila siku itakua na muhadhara mmoja.

Mhadhiri wa kozi hii ni Shekh Mahmudu Dauriyab Najafiy ameuambia mtandao wa Alkafeel kua: “Lengo la kozi hii ni kumjulisha mtafiti wa hauza au sekula misingi ya rijaliyya, kiasi cha kumpa uwelewa wa mambo haya ambayo ni muhimu sana katika sekta ya hauza”.

Akaongeza kua: “Tumewaalika wale wanao somea uhakiki na wanao penda kujua mambo haya, na sisi tunawasomesha kwa njia rahisi ili tusiwape uzito”.

Akamaliza kwa kusema kua: “Shukrani nyingi ziende kwa Atabatu Abbasiyya tukufu na kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinaadamu kwa kuwa walezi wa kozi hii ya kielimu, na kutupatia kila kitu cha lazima katika kufanikisha masomo haya”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: