Katika wiki ya kwanza ya mwezi wa Ramadhani: Idara ya ustawi wa jamii imegawa zaidi ya vikapu (700) vya chakula na mamia ya nguo kwa familia za mashahidi na masikini.

Maoni katika picha
Idara ya ustawi wa jamii ya Atabatu Abbasiyya tukufu imetangaza kua; katika wiki ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kupitia tawi lake la Bagdad imegawa zaidi ya vikapu (700) vya chakula na mamia ya nguo kwa familia za mashahidi na masikini, kwa ajili ya kupunguza japo kidogo ugumu wa maisha waliyo nayo watu hao ambao serikali haiwajali, na kutekeleza maagizo ya Marjaa Dini mkuu.

Idara imebainisha kua, ugawaji ulikua kama ifuatavyo:

  • 1- Msafara wa kuitikia wito wa Marjaiyya, ulio elekea katika mji wa Sabú-Buur chini ya kauli mbiu isemayo: (tulikuwepo tumebaki na ahadi tunatekeleza) ambako waligawa vikapu vya chakula (330) na nguo karibu (850) kwa mayatima wa Hashdi Shaábi na familia za masikini.
  • 2- Msafara wa watoto wa Marjaiyya wakazi wa mtaa wa Kafaah, waligawa vikapu vya chakula (350) kwa familia za mashahidi na masikini katika vitongoji mbalimbali vya mji wa Bagdad, kwa kufuata orodha maalum iliyokua imesha andaliwa ya watu wenye mahitaji katika mtaa wa Nasri na Sab’u-Qusuur.

Huo ndio ufafanuzi wa misaada iliyo tolewa na idara ya ustawi wa jamii ofisi ya misaada katika mji wa Bagdad ndani ya wiki ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadani.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: