Kamati ya maandalizi ya kongamano la fatwa tukufu ya kujilinda awamu ya nne yatangaza ratiba ya siku ya kwanza

Maoni katika picha
Kamati ya maandalizi ya kongamano la fatwa ya kujilinda awamu ya nne, imetangaza ratiba ya siku ya kwanza, ambayo ni siku ya Alkhamisi (23 Shawwal 1440h) sawa na (27 Juni 2019m) chini ya kauli mbiu isemayo: (Nyie ni fahari na utukufu tunajivunia katika kila umma) litakalo fanyika kwa siku mbili.

Ratiba ya siku ya kwanza itakua kama ifuatavyo:

Sehemu: Ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) ndani ya Atanatu Abbasiyya.

Muda: Saa tatu asubuhi.

  • 1- Usomaji wa Quráni.
  • 2- Wimbo wa taifa la Iraq, na wimbo wa Atabatu Abbasiyya (Lahnul-Iba).
  • 3- Ujumbe kutoka kwa kiongozi mkuu wa kisheria wa Atabatu Abbasiyya tukufu.
  • 4- Kaswida kuhusu fatwa tukufu, itakayo somwa na mshairi bwana Ali Swaffaar.
  • 5- Ujembe maalum kuhusu mauwaji ya kimbari ya (Spaika) kutoka kwa kamati ya kongamano la Spaika.
  • 6- Ujumbe kutoka katika kitabu cha fatwa tukufu ya kujilinda pamoja na kuzindua kitabu hicho.
  • 7- Ufunguzi wa maonyesho ya picha yatakayo fanyika katika eneo la katikati ya haram mbili tukufu.

Itakapo fika saa kumi na moja Alasiri:

Kutakua na warsha ya kielimu kwa anuani ya: (Khutuba za Dini na athari yake katika kupandikiza fikra za kigaidi) ndani ya ukumbi wa jengo la Imamu Haadi (a.s).

Ikifika saa mibi jioni:

Kutakua na kikao cha usomaji wa mashairi ndani ya ukumbi wa haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s).

Na mwisho kutakua na usomaji wa Quráni saa tatu usiku hapohapo ndani ya ukumbi wa haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: