Mradi wa kuku na mashine za kutotolesha mayai za kisasa… uzalishaji mkubwa

Maoni katika picha
Mradi wa kuku na mashine za kutotolesha mayai kisasa ni moja ya sekta ya uchumi ya Iraq, kutokana na mchango wake katika sekta ya chakula na kupunguza kutegemea kuku wa kuagizwa nje ya nchi, pia wanamashine za kisasa kabisa za kutotolesha mayai.

Kuhusu mradi huu tumeongea na kiongozi wa mradi wa mashine za kutotoa mayai za Alkafeel Mhandisi Dhiyaa Sharifi amesema kua: “Mradi huu ulianziswa mwaka (2016) kwa kushirikiana na watalam kutoka ulaya pamoja na watalam wa hapa nchini, nao unatumia mitambo bora na ya kisasa zaidi”.

Mmoja wa wasimamizi wa mashine za kutotolesha mayai Ustadh Abbasi Fadhili amesema kua: “Tunasambaza vifaranga katika mikoa yote ya Iraq kutokana na uwezo mkubwa wa mashine hizi katika kutotolesha mayai, kwani ni mashine za kisasa kabisa na vifaa vyake huagizwa kutoka Ulaya”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: