Dirisha la kaburi takatifu la Abulfadhil Abbasi (a.s) ni pambo bora miongoni mwa mapambo ya kiislamu ya kisasa

Maoni katika picha
Dirisha la kaburi la Abulfadhil Abbasi (a.s) limepambwa vizuri kwa mapambo ya kiislamu ya kisasa, limeandikwa hati nzuri za kiarabu zilizo chimbwa katika mbao na zilizo nakshiwa kwa dhahabu na fedha halisi.

Herufi hizo zimeandikwa kwa hati ya (Thuluth Jalliy), ambayo ni moja ya hati halisi za kiiraq iliyo anzishwa katika zama za utawala wa bani Abbasi, zimeandikwa na mikono ya wairaq inayo watii na kuwapenda watu wa nyumba ya Mtume (s.a.w.w).

Kumbuka kua dirisha la myweshaji wenye kiu Karbala (a.s) huzingatiwa kua dirisha lenye mapambo ya pekee, yaliyo tengenezwa kwa mikono ya wairaq wazalendo waliojitolea kumtumikia Abulfadhil Abbasi (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: