Kituo cha Dirasaat Afriqiyya chatangaza shindano la kitafiti na chatoa wito kwa wasomi na watifiti washiriki katika shindano hilo

Maoni katika picha
Kituo cha Dirasaat Afriqiyya chini ya kitengo cha habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya kimetangaza shindano la utafiti bora, na kimetoa wito kwa wasomi na watafiti kushiriki katika shindano hilo, mwisho wa kupokea tafiti za washiriki ni (15 Novemba 2019m), kisha utafanyika ushindinishaji wa tafiti na kupata zitakazo shinda na (20 Desemba 2019m) washindi watakabidhiwa zawadi zao.

Mada zinazo shindaniwa:

  • 1- Adabu (Harakati za adabu na nafasi yake katika kusambaza utamaduni wa Ahlulbait (a.s) katika bara la Afrika).
  • 2- Somo la Quráni katika zama hizi na upeo wa usasa katika bara la Afrika.
  • 3- Hadithi tukufu na wanahadithi wa kiafrika.. juhudi na historia.
  • 4- Muingiliano wa kiitikadi baina ya Dini, makundi na miji ya kiafrika.
  • 5- Uhalisia wa milengo ya kidini katika bara la Afrika na mwitikio wake kwenye jamii za kiafrika.

Masharti ya shindano:

  • 1- Utafiti utokane na mada zilizo tangazwa, na mtafiti abainishe mada anayo andika.
  • 2- Utafiti usiwe umeshawahi kutumika kwenye shindano lingine au kuchapishwa mahala pengine.
  • 3- Tafiti zitawasilishwa kwenye kamati ya majaji, na hawalazimiki kurudisha tafiti zitakazo kosa sifa ya kushiriki kwa wahusika.
  • 4- Utafiti usiwe chini ya kurasa (15) wala usizidi kurasa (35) kwa ukubwa wa (sm 2.5) kila upande, na hamishi ya (sm 3.5) upande wa kulia.
  • 5- Uandikwe kwa lugha ya kiarabu salama, ukubwa wa hati uwe (14), aina ya hati iwe (Traditional Arabic) na uandikwe kupitia program ya (word).
  • 6- Kwenye karatasi ya juu (jalada) muandishi aandike jina la mada iliyo fanyia utafiti, jina lake kamili, sehemu anayo fanyia kazi na jina la nchi.
  • 7- Mtafiti anatakiwa kuzingatia kanuni za tafiti za kielimu kwa kuangalia uhalisia wa mambo, asiandike kama hadithi ya incha, na anatakiwa kutaja vitabu rejea na majina ya waandishi wa vitabu hivyo.
  • 8- Utafiti usiwe umefutwa futwa, kiwango cha ufutaji kisizidi asilimia ishirini (%20).
  • 9- Kituo hakiwajibiki kurudisha tafiti kilizo pokea kwa wahusika.
  • 10- Upokeaji wa tafiti umeanza (16/09/2019m) hadi (20/11/2019m) kupitia parua pepe ifuatayo: africancenter22@gmail.com
  • 11- Tafiti zitaandikwa katika jarida la (Dirasaat Afriqiyya).

Kwa maelezo zaidi piga sim (07801020562).

Zawadi za washindi ni:

  • Mshindi wa kwanza: $1000 dola za kimarekani.
  • Mshindi wa pili: $800 dola za kimarekani.
  • Mshindi wa tatu: 500 dola za kimarekani.
  • Zawadi saba za wanaofuata: $100 dola za kimarekani.
  • Vyeti ya ushiriki kwa wote watakao shiriki.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: