Kitengo cha eneo la katikati ya haram mbili tukufu kinasaidia kuongoza matembezi ya mazuwaru na mawakibu

Maoni katika picha
Kitengo hicho ni sawa na vitengo vingine vya Ataba mbili tukufu Husseiniyya na Abbasiyya, watumishi wa kitengo cha katikati ya haram mbili katika ratiba yao ya ziara ya Arubaini, wanasaidia kuongoza mazuwaru na mawakibu kutokana na msongamano mkubwa uliopo katika uwanja wa katikati ya haram mbili na maeneo ya karibu la malalo mbili tukufu.

Miongoni mwa kazi zinazo fanywa na kitengo hicho kwa mujibu wa maelezo ya Sayyid Mussawi ni:

  • - Kuweka waelekezaji katika eneo la uwanja wa katikati ya haram mbili na maeneo yanayo zunguka malalo mbili tukufu kwa ajili ya kuongoza mazuwaru na kuwaelekeza sehemu wanazo hitaji.
  • - Kuweka mageti ya muda yanayo hamishika kwa ajili ya kukagua mazuwaru na mawakibu.
  • - Kuratibu uingiaji na utokaji wa mazuwaru na mawakibu katika haram mbili tukufu.
  • - Kutenga sehemu maalum ya kupumzika wanawake na sehem ya wanaume kwa ajili ya kuondoa mchanganyiko usio faa baina yao.
  • - Kuratibu uingiaji na utokaji wa vifaa vya usafiri katika eneo la katikati ya haram mbili.

Akabainisha kua: “Kazi zote hizo zinafanywa na watumishi wa idara hiyo pamoja na wafanyakazi wa kujitolea, wanafanya kazi usiku na mchana”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: