Mawakibu za kutoa misaada zipo katika viwanja vya maandamano kuwasaidia watu wanaofanya maandamano ya amani na kudai haki zao kisheria.

Maoni katika picha
Kama ilivyo simama imara kusaidia wapiganaji wa Hashdi Shaábi wakati na baada ya vita na Daesh, leo idara ya ustawi wa jamii chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu kupitia mawakibu zake kutoka mikoa mbalimbali zinashiriki kutoa misaada kwa watu wanaofanya maandamano ya amani na kudai haki zao kisheria, walizo pewa na katiba na kuungwa mkono na Marjaa Dini mkuu, wanafanya kazi bega kwa bega na mawakibu zingine za Husseiniyya.

Idara imesema kua tangu yalipo anza maandamano imekua mstari wa mbele kusaidia waandamanaji, ilianza kufanya hivyo katika uwanja wa uhuru huko Bagdad, kisha wakaenea kwenye mikoa mingine, miongoni mwa huduma wanazo toa ni:

  • - Kujenga vituo vya kutoa huduma.
  • - Kuandaa chakula na kukigawa kwa waandamanaji.
  • - Kugawa chakula, maji na juisi kwa waandamanaji.
  • - Kutoa huduma za matibabu kwa majeruhi.
  • - Kuandaa gari za wagonjwa na kutoa huduma ya kwanza ya matibabu.
  • - Msaada wa kimkakati na kuhakikisha mawakibu nyingi zinakuwepo katika uwanja wa maandamano.
  • - Kugawa baadhi ya vifaa vinavyo tumiwa na waandamanaji.
  • - Kushiriki katika makundi ya kujitolea kufanya usafi na kazi zingine.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: