Sauti ya raia: Haya yalisemwa na Marjaa Dini mkuu tarehe (21/10/2011m).

Maoni katika picha
Kwa muda mrefu Marjaa Dini mkuu amekua akisisitiza umuhimu wa kufanya mabadiliko (islahi), yanayo weza kutatua changamoto za raia wa Iraq, katika sekta ya siasa, uchumi na zinginezo.

Katika khutuba ya Ijumaa (22 Dhulqadah 1432h) sawa na (21/10/2011m) iliyo tolewa na Mheshimiwa Shekh Abdulmhadi Karbalai ndani ya haram ya Imamu Hussein (a.s), alieleza mambo kadhaa muhimu na matarajio ya wananchi wa Iraq, miongoni mwa mambo hayo ni:

  • 1- Matumizi ya pesa yaelekezwe kwenye kujenga nyumba za makazi, jambo hilo litasaidia kuboresha huduma kwa raia.
  • 2- Kuwatumia watalamu wasiokua na ajira katika miradi inayo hitajiwa na raia.
  • 3- Kuboresha sekta ya viwanda, kilimo, utumishi, utalii na zinginezo.
  • 4- Kuwa na utashi thabiti na maamuzi imara ya kupambana na ufisadi katika vyama vya kisiasa.
  • 5- Tunahitaji kurekebisha taratibu za kiutawala kwa kufanyia marekebisho sheria za zamani na kuondoa vipengele vinavyo kwamisha maendeleo na kuzuwia wawekezaji kuja Iraq.
  • 6- Lazima kuwe na utaratibu wa wazi na adilifu katika uteuzi wa nyadhifa serikalini, wala sio kwa ujamaa na undugu.
  • 7- Kipaombele iwe kupunguza ufakiri Iraq hasa kwa wajane na mayatima, watu ambao wanaongezeka kila siku kutokana na matatizo yanayo endelea hapa nchini.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: