Chuo kikuu cha Al-Ameed chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu kimeanza kufanya program ya maelekezo ya kielimu, yanayo husu kuandaa kumbi maalum za kufundishia (madarasa), nayo ni miongoni mwa program zinazo lenga kufikia lengo la kujiepusha na hatari yeyote inayo weza kutokea kielimu.
Program hii inafanywa chini ya kauli mbiu isemayo: (mazingira salama ya kujisomea) ilianza kutekelezwa mwaka jana, na itaendelea miaka mitano ijayo kwa mujibu wa ratiba yake.
Kaulimbiu tajwa inabeba dhana ya maelekezo ya kielimu, inaruhusu kanuni ya maandalizi na uhakiki wa ratiba pamoja na mambo mengine.