Kitivo cha udaktari katika chuo kikuu cha Al-Ameed chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu, kimetoa mhadhara wa kielimu usemao: (matatizo ya damu na utambuzi wake) kwa kushirikiana na idara ya afya ya mkoa wa Karbala/ hospitali kuu ya Ainu-Tamru chini ya ratiba ya elimu endelevu katika chuo.
Muhadhara huo umetolewa na Dokta Rahim Mahadi Rahim, na kuhudhuriwa na kundi kubwa la wakufunzi wa chuo pamoja na madaktari kutoka idara ya afya ya mkoa wa Karbala.
Amezungumzia matatizo ya damu na sababu zake pamoja na njia za kuyatambua. Kumbuka kua chuo cha Al-Ameed hufanya nadwa na warsha za kielimu katika kipindi chote cha mwaka kwa ajili ya kuwaimarisha zaidi kielimu wanafunzi wake.