Mada nne kwa juzuu sita: zimejaa wema wake

Maoni katika picha
Kitengo cha masomo ya kitafiti kwa Abulfadhil Abbasi (a.s) chini ya maktaba na Daru Makhtutwaat ya Atabatu Abbasiyya kimeandika mada nne katika juzuu sita kuhusu Abulfadhil Abbasi (a.s), mada hizo ni:

  • Abulfadhil Abbasi (a.s) katika mashairi ya kiarabu/ juzuu la nne, (yalitolewa majuzuu matatu).
  • Nibrasu Anwaru fi Abbasi Akbaru.
  • Abbasi mtoto wa kiongozi wa waumini (a.s) na malalo yake tukufu katika vitabu vya safari za waarabu vilivyo tafsiriwa.
  • Atabatu Abbasiyya katika nyaraka za Iraq/ sehemu ya kwanza: ujenzi wa mwaka 1921-1992.

Mkuu wa kituo hicho Shekh Mahmudu Swafi ameuambia mtandao wa Alkafeel kua: “Tangazo la vitabu hivi limetolewa katika nadwa iliyo ratibiwa na kituo, na kuhudhuriwa na jopo la wabobezi wa mambo hayo, wamejadili kitabu hicho na kukitambulisha, pamoja na kutambulisha kazi za kituo na machapisho yake makuu sambamba na mipango yake ya baadae, na kufungua milango ya kusaidiana na kila anayependa”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: