Kwa video: chuo kikuu cha Al-Ameed kinafanya kikao cha kwanza na wanafunzi waliopata nafasi za kwanza.

Maoni katika picha
Atabatu Abbasuyya tukufu inatilia umuhimu sana swala la kuboresha kiwango cha elimu hapa Iraq, na kuwepo kwa uhusiano wa elimu na maarifa katika jamii, kupitia taasisi zake za malezi na elimu kikiwemo chuo kikuu cha Al-Ameed, kinacho julikana kwa kufuata mlengo bora wa wakisasa na kimataifa.

Chio kimefanya mkutano wa kwanza na wanafunzi waliopata nafasi za kwanza pamoja na wazazi wao, kwa ajili ya kubainisha maazimio ya mwaka wa masomo, na kuweka mikakati inayo endana na wanafunzi, sambamba na kuchukua mazingatio kutokana na hali ya taifa kwa sasa.

Makamo kiongozi mkuu wa mambo ya wanafunzi katika kitivo cha udaktari wa meno, Dokta Rahim Mahadi amesema kua: “Tunafuatilia kwa karibu maendeleo ya vyuo kielimu, hivyo tumeweka mikakati ya kunufaika na vipindi vya likizo kwa kuwafundisha wanafunzi masomo yaliyo wapita na kuhakikisha wanaweza kusoma mada zote za lazima kwa mwaka”.

Tambua kua chuo kikuu cha Al-Ameed kimejikita katika misingi ya elimu inayo endana na mazingira pamoja na wanafunzi wa sasa, ili kufikia mahitaji ya taifa.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: